Free Palestine

Free Palestine
Showing posts with label Hamas. Show all posts
Showing posts with label Hamas. Show all posts

Saturday, November 17, 2012

WAZAYUNI (ISRAEL) WAENDELEZA MASHAMBULIZI UKANDA WA GAZA


Wapalestina wasiopungua wanne wameuawa shahidi baada ya ndege za utawala wa Kizayuni wa Israel usiku kushambulia maeneo kadhaa ya Ukanda wa Gaza. Ashraf al Qudwa Msemaji wa Wizara ya Afya ya serikali halali ya Palestina inayoongozwa na Hamas amesema kuwa, kombora la ndege ya Israel ilikita katika nyumba ya familia ya Abu Jalal, na kupelekea watu wanne wa familia hiyo kuuawa shahidi. Ameongeza kuwa, tokea yaanze mashambulizi ya kinyama ya Wazayuni huko Gaza siku ya Jumatano hadi sasa, zaidi ya watu 30 wameuawa shahidi na wengine 270 kujeruhiwa. Wakati huohuo, jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel umekiri kuangushwa ndege ya kijeshi F16 katika anga ya Gaza. Brigedi ya Izzuddin Qassam tawi la kijeshi la HAMAS ilitangaza jana usiku kwamba ilitungua ndege ya kijeshi ya Israel katika eneo la magharibi mwa Ukanda huo. Kwa upande mwengine, William Hague Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Uingereza ameitahadharisha Israel juu ya kuendeleza mashambulizi yake huko Gaza, na kusisitiza kuwa, bila shaka mashambulizi hayo yatakuwa na mwisho mbaya kwa utawala huo. Hague ameongeza kuwa, mashambulizi hayo yatapelekea Israel kukosa uungaji mkono wa jamii ya kimataifa. Hata hivyo, Hague ameshindwa kulaani jinai za majeshi ya Israel na badala yake amelaani mashambulizi ya roketi yaliyofanywa na wanamapambano wa Kipalestina dhidi ya vitongoji vya Israel.

AMIR WA QATAR ATUHUMIWA KUWAUZA HAMAS


Duru za kuaminika zinasema kuwa, safari iliyofanywa hivi karibuni na Sheikh Hamad bin Khalifa al Thani Amir wa Qatar katika eneo la Ukanda wa Gaza, ilifichua makazi ya viongozi kadhaa wa ngazi za juu Hamas. Kwa mujibu wa Shirika la Habari la FARS NEWS, Sheikh Hamad bin Khalifa al-Thani aliwapa viongozi wote wa ngazi za juu wa Hamas zawadi za saa za mkononi na kalamu ambazo ndani yake mulikuwa na zana zilizokuwa zikiwasiliana na satalaiti za utawala wa Kizayuni wa Israel na kuwasaidia kuonyesha nyendo zao na mahala wanapoishi viongozi hao. Ahmad al Ja'abari mmoja kati ya makamanda wa ngazi za juu wa Izzuddin Qassam aliyeuawa shahidi siku chache zilizopita, alilengwa na ndege za kivita za Israel baada ya kufuatiliwa nyendo zake kwa usaidizi wa saa na kalamu alizopewa zawadi na Amir wa Qatar. Kwa upande mwengine, imeelezwa kuwa, Amir wa Qatar amemueleza wazi Ismail Haniya Waziri Mkuu wa serikali iliyochaguliwa na wananchi wa Palestina inayoongozwa na Hamas kwamba, kama wanataka misaada ya kifedha kutoka Qatar, wanapaswa kuacha kushirikiana na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na wakati huhuo wautambue rasmi utawala wa Kizayuni wa Israel. Aidha Amir wa Qatar alitoa masharti matano kwa Harakati ya Hamas ili iweze kupata misaada ya kifedha na kiuchumi kutoka Qatar, ikiwa ni pamoja na kuacha kushirikiana na Iran, kuanzisha mazungumzo na utawala wa Kizayuni wa Israel bila ya masharti, kuutambua rasmi utawala wa Kizayuni wa Israel, kuitambua Quds Tukufu kuwa ni mji mkuu wa utawala huo ghasibu na kuacha kabisa muqawama na mapambano ya kutumia silaha.

HAMAS YATUNGUA NDEGE YA ISRAEL HUKO PALESTINA


Wanamapambano wa Palestina wametungua ndege ya kijeshi ya utawala wa Kizayuni wa Israel iliyokuwa inafanya mauaji dhidi ya wananchi wa Palestina.

Televisheni ya al Quds imezinukuu Brigedi za Izuddin Qassam, tawi la kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Palestina HAMAS zikisema kuwa, ndege za utawala wa Kizayuni zimefanya mashambulizi makali katika eneo ilipoanguka ndege hiyo ya Israel ili kufuta ushahidi na kuwazuia wanamapambano wa Palestina wasipate mabaki ya ndege hiyo.

Vile vile wanamapambano wa Palestina wamefanikiwa kwa mara ya kwanza kushambulia maeneo ya Wazayuni katika mji wa Baytul Muqaddas na kuzusha kiwewe katika safu za utawala wa Kizayuni.

Kabla ya hapo pia HAMAS ilikuwa imetungua ndege ya Israel isiyo na rubani na ilishambulia pia Tel Aviv mji mkuu wa utawala wa Kizayuni na kuwalazimisha viongozi wa Israel wakimbilie mafichoni.

Televisheni ya al Quds imetangaza pia kuwa wanapambanao wa Palestina wamelishambulia kwa kombora bunge la utawala wa Kizayuni, Knesset, huko magharibi mwa Baytul Muqaddas. Taarifa zinasema pia kuwa hoteli za kitalii za Wazayuni zimefungwa huko Baytul Muqaddas baada ya maeneo yanayokaliwa kwa mabavu na Wazayuni ya mji huo kushambuliwa kwa makombora ya wanamapambano wa Palestina.