Free Palestine

Free Palestine

Thursday, January 19, 2012

MFALME WA QATAR AFANYA ZIARA YA SIRI ISRAEL + VIDEO


Mfalme wa Qatar, Sheikh Hamad bin Khalifa Aal Thani amefanya ziara ya siri ya kuutembelea utawala wa Kizayuni licha ya uhakika kwamba Qatar haina uhusiano wa kisiasa na Israel.

Mkanda mmoja wa video unamuonesha Amir huyo wa Qatar pamoja na Waziri Mkuu wake Sheikh Hamad bin Jasim bin Jabir Aal Thani wakikaribishwa na Tzipi Livni, mkuu wa chama cha Kadima cha Israel.

Mfalme huyo wa Qatar ameonana pia na maafisa wengine kadhaa wa ngazi za juu wa utawala wa Kizayuni wa Israel.
Kuwekwa mkataba mpya wa gesi kati ya Doha na Tel Aviv ni miongoni mwa masuala muhimu yaliyojadiliwa katika ziara hiyo ya Amir wa Qatar na ujumbe wake mzito huko Israel.


Qatar imeweka mkataba mpya wa gesi na Israel baada ya mkataba wa gesi kati ya utawala wa Kizayuni na Misri uliokuwa umewekwa wakati wa utawala wa dikteta Hosni Mubarak kuingia hatarini kufuatia wanaharakati wa Kiislamu kupata ushindi mutlaki katika uchaguzi wa hivi karibuni wa Bunge nchini Misri na ambao ulikuwa wa kwanza tangu kupinduliwa kibaraka mkubwa wa nchi za Magharibi, Hosni Mubarak.

Wednesday, January 18, 2012

zaidi ya wanafunzi 1000 wa Kiirani wameomba kubadilisha taaluma zao kuelekea taaluma ya Fizikia na Uhandisi wa Nishati ya Nyuklia


Waziri wa Elimu, Teknolojia na Utafiti wa Iran Kamran Daneshjoo ametangaza kwamba zaidi ya wanafunzi 1000 wameomba kubadilisha taaluma zao kuelekea taaluma ya Fizikia na Uhandisi wa Nishati ya Nyuklia.

Daneshjoo amesema, wanafunzi wapatao 300 wa Chuo Kikuu cha Ufundi cha Sharif na vilevile wanafunzi zaidi ya elfu moja wa muhula wa kwanza wa masomo katika vyuo vikuu nchini wameomba kubadilisha taaluma zao ili kusomea fani ya Fizikia na Uhandisi wa Nishati ya Nyuklia.

Amesema jambo hili linaashiria kwamba mbinu za mauaji zinazofanywa na maadui dhidi ya wasomi wa Nyuklia wa Iran hazina taathira yoyote ya kuwatia woga wanafunzi hao, na kwamba mbinu hizo hazikuwasaidia lolote maadui hao.

Ameashiria kwamba kwa mujibu wa takwimu mpya zilizotolewa na mtandao wa Kielimu wa Kimataifa "Escobos" Iran imejipatia nafasi ya kwanza katika upande wa elimu, wakati ambao ilikuwa ya pili baada ya Uturuki.

Waziri huyo ameongeza kwamba idadi ya wanafunzi wa Vyuo Vikuu imefikia milioni nne huku idadi ya waliochaguliwa ikizidi pia, na amesema kwamba wakuu wa vyombo vya usalama wanafanya juhudi kubwa usiku na mchana katika kuhakikisha maisha ya wanafunzi hao yanakuwa salama kutokana na njama mbaya za maadui.

Jumuiya ya NAM yaalani hatua ya Marekani ya kukiuka anga ya Iran


Jumuiya ya Nchi Zisizofungama na Siasa za Upande Wowote NAM imelaani ukiukaji wa anga ya Iran uliofanywa na ndege ya ujasusi ya Marekani isiyo na rubani mwishoni mwa mwaka jana. Kitengo cha mawasiliano cha jumuiya ya NAM kimetoa taarifa kikilaani ukiukaji huo uliofanywa na ndege ya ujasusi ya Marekani isiyo na rubani katika anga ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Jumuiya ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote NAM ambayo ina wanachama 120 imeeleza katika taarifa yake kuwa, ukiuaji wa anga ya Iran ni kinyume na sheria zote za kimataifa zinazohusiana na mamlaka ya kujitawala ya anga za nchi mbalimbali. Mapema mwezi huu Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC pia ilikemea hatua hiyo ya ndege ya ujasusi ya Marekani ya kuingia katika anga ya Iran kinyume cha sheria. Disemba 4 mwaka jana Iran ilitangaza kuwa kitengo chake cha masuala ya kielektoroniki katika vikosi vya jeshi kimefanikiwa kuidhibiti ndege hiyo ya ujasusi ya Marekani aina ya RQ-170 Sentinel ambayo ilikuwa ikipaa katika anga ya mji wa Kashmar huko kaskazini magharibi mwa Iran na baadae kuishusha chini.

Tuesday, January 17, 2012

UKOSEFU WA UADILIFU WAONGEZEKA KATIKA NCHI TAJIRI DUNIANI


Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani WHO amesema kuwa ukosefu wa uadilifu wa kijamii katika nchi tajiri ulimwenguni unazidi kuongezeka.

Bi Margaret Chan, raia wa China, alisema hayo jana katika kikao cha WHO kilichofanyika mjini Geneva Uswisi na kuongeza kuwa, ukosefu huo wa uadilifu katika baadhi ya nchi tajiri duniani unashuhudiwa zaidi katika hali ya maisha baina ya watu wazee na vijana.

Dk. Chan ameongeza kuwa, ukosefu wa uadilifu katika kipato cha watu wa nchi hizo tajiri ni mkubwa mno kiasi kwamba haujawahi kushuhudiwa mfano wake katika kipindi cha miaka 25 iliyopita.
Ukosefu wa uadilifu unaongezeka pia baina ya nchi na nchi na baina ya mataifa tajiri na mataifa maskini duniani, huku mataifa ya kibepari yakizidi kuzinyonya nchi changa ulimwenguni.

Dk. Margaret Chan amesema pia kuwa idadi ya vifo vya watoto wadogo iliongezeka sana mwaka 2011 idadi ambayo haijawahi kushuhudiwa mfano wake katika kipindi cha miaka 60 iliyopita.


Monday, January 16, 2012

EXPERTS CALL FOR ENERGY DRINK WARNINGS


The Australian Medical Association calls for age-restrictions on energy drinks following significant rise in the number of teens affected by adverse effects.

Health experts from the University of Sydney and the New South Wales Poisons Information Centre warned that reports of reactions caused by drinks such as Red Bull and V jumped from just 12 in 2004 to 65 in 2010. 

According to their report published in the Medical Journal of Australia, during the 7 years period 297 calls for assistance were recorded with at least 128 people hospitalized due to over-consumption of the highly caffeinated drinks. 

The symptoms included heart palpitations, agitation and stomach upsets and even seizures and hallucinations in some cases. 

The median age of people who were affected by the drinks was 17 years and more among those who mixed energy drinks with alcohol. 

“Given the clear evidence of toxicity and the growing number of hospitalizations associated with consumption of energy drinks, particularly in a vulnerable adolescent population, health authorities should increase awareness of the problem, improve package labeling and regulate caffeine content,” experts noted. 

They suggested that energy drinks should carry warning labels similar to those for non-prescription, over-the-counter caffeine tablets. 

The request has already been rejected by the Australian Beverages Council representing energy drink industry by saying that the country has the strongest regulation of all world markets.